Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani 2023: Amani na Ustawi

Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani 2023: Amani na Ustawi

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani tarehe Saba, Mwezi Julai 2023 ni “Kiswahili kwa Amani na Ustawi.” Lengo kuu la maadhimisho haya ni kusaidia kunogesha matumizi ya lugha ya Kiswahili kama nguvu ya amani, ustawi na maendeleo endelevu ya binadamu sanjari na mchakato wa kuimarisha tamaduni mbalimbali. Siku hii ilianzishwa na UNESCO tarehe 23 Novemba 2021 na kuanza kuadhimishwa tarehe 7 Julai 2022. Leo tunayo Historia ya Kiswahili.

Idara ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Nairobi kilishiriki katika hafla hiyo kikamilifu.