Profesa Iribe mwenyekiti wa Idara ya kiswahili pamoja na wenyekiti wa idara mbalimbali katika Mahafala ya tarehe 16 Disemba 2022
Mwandishi wa Sauti ya Dhiki Abdilatif Abdallah aliitembelea Idara mnamo tarehe 21 Novemba, 2022.
Alipokelewa vyema na Prof. Iribe, mwenyekiti wa idara ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Nairobi.
Idara ya Kiswahili iliwezesha wanafunzi wanane wa uzamili na wanne wa uzamifu kufuzu tarehe 16 Desemba 2023. Wazamifu waliofuzu ni pamoja na;
1. Dkt. Josphat Gitonga
2. Dkt. Sanja Leonard
3. Dkt. Silas Thuranira (aliaga dunia siku chache kabla ya mahafala)
4. Dkt. Rose Kawira
Mwenyekiti wa Idara Prof Iribe Mwangi siku ya Mahafala tarehe 16 Desemba
Prof. Iribe Mwangi, mwalimu wa Kiswahili ni miongoni mwa Wakenya 460 waliotuzwa na Rais William Ruto katika sherehe za Kitaifa za 59 za jamuhuri.
Profesa Iribe ni ni mwenyekiti wa Idara ya Kiswahili chuo kikuu cha Nairobi. Aliweza kutunukiwa tuzo ya Head of State Commendation (HSC) kwa mchango wake katika makuzina maendeleo ya Kiswahili ambayo yameathiri sera ya lugha nchini Kenya.
Darasa la Kiswahili Nchini Malawi ni sehemu ya Jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ubalozi wake Nchini Malawi kukipeleka kiswahili nje kama Lugha, utamaduni na bidhaa. Darasa la kwanza limeendeshwa na Wataalam wa kiswahili kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na baadaye darasa hilo litaendelezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo Kikuu cha Hebron cha Nchini Malawi.
Wabunge wanasema ni wakati kwa Kenya kubuni baraza la kitaifa la kiswahili, kusaidia kuipa lugha hii hadhi inayostahiki. Wabunge waliokuwa wakichangia hoja ya mbunge wa Kamukunji Yusuf Hassan walisema kuwa, kuimarishwa kwa utumizi na hadhi ya kiswahili kutasaidia kuimarisha utangamano zaidi, sio tu hapa nchini na kanda ya Afrika Mashariki, bali pia dunia nzima ambapo lugha hii inaenziwa.