Saba Saba: Maadhimisho Ya ‘Siku Ya Kiswahili Duniani’ Jijini Nairobi

Mwinyimsa alijuzwa kwangu mkereketwa mkubwa wa Kiswahili, Wambugu Yusuf. Wote wawili waliniuliza swali, “Prof, kuna mipango ipi kuhusu maadhimisho ya siku ya Kiswahili?” Niliwajibu nilivyowezeshwa.

Siku iliyofuata Henry Indindi, mwanafunzi wangu wa zamani kama vile Yusuf, aliniuliza swali lilo hilo na jana, Jackton Nyonje, alitaka kujua kama kuna mipango yoyote ya kuadhmisha. Inadhihirika kwangu kwamba kuna wengi wanaojiuliza swali hili na kwa sababu hiyo naona bora kutoa maelezo machache nilioyonayo hapa, japo kwa kifupi.