In the 1950s the United Nations established the Kiswahili language unit of United Nations Radio, and today Kiswahili is the only African language within the Directorate of the Global Communications at the United Nations. The United Nations General Assembly, through its https://www.youtube.com/watch?v=JViGHXhu_t4
Mwinyimsa alijuzwa kwangu mkereketwa mkubwa wa Kiswahili, Wambugu Yusuf. Wote wawili waliniuliza swali, “Prof, kuna mipango ipi kuhusu maadhimisho ya siku ya Kiswahili?” Niliwajibu nilivyowezeshwa.
Siku iliyofuata Henry Indindi, mwanafunzi wangu wa zamani kama vile Yusuf, aliniuliza swali lilo hilo na jana, Jackton Nyonje, alitaka kujua kama kuna mipango yoyote ya kuadhmisha. Inadhihirika kwangu kwamba kuna wengi wanaojiuliza swali hili na kwa sababu hiyo naona bora kutoa maelezo machache nilioyonayo hapa, japo kwa kifupi.