Darasa la Kiswahili Nchini Malawi ni sehemu ya Jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ubalozi wake Nchini Malawi kukipeleka kiswahili nje kama Lugha, utamaduni na bidhaa. Darasa la kwanza limeendeshwa na Wataalam wa kiswahili kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na baadaye darasa hilo litaendelezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo Kikuu cha Hebron cha Nchini Malawi.