WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UKUAJI WA KIBIASHARA
OFISI YA KATIBU WA WIZARA
Kuanzia mwezi Juni 2020 hadi Juni 2021, Chuo Kikuu cha Nairobi kinaadhimisha miaka 50 tangu kuasisiwa kwake. Kumekuwa na shughuli nyingi hasa webina za kiusomi ambazo zimekuwa zikiendelea na zitaendelea hadi Juni 2021. Idara ya Kiswahili tayari imekwishaandaa webina iliyokuwa na kaulimbiu ya “Kiswahili Ulimwenguni.” Hata hivyo, kilele cha sherehe hizi kitakuwa Alhamisi tarehe 10 Desemba 2020 kuanzia saa nane alasiri.
Sherehe hizi zitafanyika mnamo tarehe 11 Desemba kuanzia saa mbili asubuhi. Sherehe hizi zitafanyika kupitia mtandao kutokana na janga la Korona. Kati ya watakaofuzu ni wazamifu 66. Hii ni sherehe ya pili kufanyika kwa njia ya mtandao huku ya kwanza ikifanyika tarehe 25 Septemba, 2020. Ndaki yetu ya Insia na Sayanzi za Jamii ndiyo itakayokuwa na washiriki wengi kabisa.
• AFISA MKUU MTENDAJI WA TUME YA ELIMU YA
VYUO VIKUU, PROF. MWENDA NTARANGWI,
Siku Jumatano tarehe 2, Disemba, 2020, Idara ya Kiswahili kupitia kamati andalizi, iliandaa webina kusherehekea miaka 50 tangu Chuo Kikuu cha Nairobi kilipoanzishwa rasmi. Kauli Mbiu ya webina ilikuwa, “Kiswahili Ulimwenguni.”