Latest News & Announcements

Webina ya Idara ya Kiswahili

Kama sehemu ya maadhimisho ya jubilee ya miaka hamsini, idara ya Kiswahili kupitia kamati andalizi  imeandaa Webina yenye mada kuu; Kiswahili Ulimwenguni.

Hafla hiyo itafanyika Desemba 2, 2020 kwanzia 2.00 mchana hadi 5.30 jioni. Mfunguzi wa hafla hiyo ni Makamu mkuu wa Chuo, Profesa Stephen Kiama.  Makala Elekezi yatajadiliwa na  Prof. Mwenda Ntarangwe, kutoka Tume ya Elimu ya Vyuo Vikuu. Mwasilishaji wa makala maalum ni Prof. Ngugi wa Thiong’o, Chuo Kikuu cha California, Irvine.

KUBIDHAISHA KISWAHILI

Nchi ya Kenya imekuwa mbioni kujiandaa kibiashara katika siku za usoni. Ari ya kujiandaa kibiashara imechocewa na mambo mawili muhimu: Kwanza, Sheria ya Ukuaji na Fursa Barani Afrika (AGOA), mpango wa upendeleo, unafika kikomo mwisho wa mwaka 2025.  Kwa sababu hii, nchi ya Kenya inapanga mikakati yake ya biashara baada ya 2025. Hata hivyo, mazungumzo yake yanakaribisha nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Renowned Kenyan Poet Abdalla Mwasimba Passes on!

The Swahili literary world was yet again thrown into mourning Wednesday, following the death of legendary poet Abdalla Mwasimba aged 83.

His death occurred a few months after Ken Walibora, Abdalla Shamte and Euphrase Kezilihabi.

Mwasimba, who for close to 30 years revised Swahili poems for Taifa Leo, had been suffering from low blood pressure and diabetes.

His youngest son, Mwasimba Abdallah told the Nation that the poet died in his sleep at his granddaughter’s residence in Kaloleni, Nairobi.

KONGAMANO LA 6 LA KIMATAIFA, CHUO KIKUU CHA PWANI KILIFI, KENYA

Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) kimeandaa kongamano la 6 la kimataifa katika Chuo Kikuu cha Pwani Kilifi, Kenya mnamo tarehe 15-17 Dis. 2020

Mda wa makataa ya ikisiri uliongezwa hadi Tarehe 30 Juni, 2020. Wapenzi na wasomi wa Kiswahili wanaombwa kutuma ikisiri kabla au kufikia tarehe ya makataa.

Taarifa zaidi kuhusu CHAUKIDU zimo katika kiambatisho.

 

MKUTANO WA IDARA YA KISWAHILI ULIOFANYIKA KUPITIA MTANDAO TAREHE 6 APRILI 2020

Huu ni mkutano wa kwanza uliofanyika kupitia mtandaoni. Ajenda kuu zilikuwa ; mawasiliano kutoka kwa Mwenyekiti; Makaribisho ya walimu wapya;  Livu ya mwaka, Utahini wa tasnifu za uzamifu; Usimamizi wa tasnifu za uzamili na uzamifu; Ufundishaji wa wanafunzi wa MA, BA na BED na maswala mengineyo.

Hoja kuu kutoka kwa mkutano huo ni pamoja na; wwenyekiti kuhimiza walimu kutumia mtandao kuwafikia wanafunzi wanaofundishwa kutumia njia mbalimbali zilizomo k.v Zoom, WhatsApp na kadhalika.